

Katika hali isiyo ya kawaida hivi karibuni msanii wa maigizo Wastara Juma aliyewahi kutamba na filamu ya Mboni yangu, 2Brothers, Round, Vita Mkomanae, alipigiwa simu na moja kati ya namba hizo ambazo hazieleweki hivyo alimtaarifu mumewe Juma Kilowoko juu ya simu hiyo. ndipo mumewe alipokurupuka na kumpokonya simu mkewe na kumkataza asije akaipokea kwani anaweza kupoteza maisha au kupararaizi
Ingawa Wastara hakuonesha kuamini maneno hayo na kudai kuwa alitarajia kupokea simu kutoka nje ya nchi hivyo mara nyingi simu za kutoka nje huwa hazionyeshi namba ya mpigaji bali huwa inaonekana 'private no' or 'unknown call' hivyo kusababisha mabishano baina ya wapendanao hao wawili na mwisho kufikia muafaka wa kutoipokea simu hiyo...