TICO EDITOR

Monday, September 20, 2010

BAADA YA DAMALISA SASA NI HIDEN TRUTH

Baada ya filamu ya DAMALISA kuingia sokoni na kupokelewa vizuri na mashabiki wa filamu za kutisha, sasa AKIM NATIBU ambaye ndiye aliyeiproduce filam hiyo ya DAMALISA, anaandaa filamu nyingine ambayo anatarajia itakuwa bomba kuliko DAMALISA.

Pia filamu hiyo ambayo ameipa jina la HARD TIME (Ukweli uliofichika), inatarajia kuanza kurekodiwa mara ifikapo mwezi 11 mwaka huu, "ni matarajio yangu kuwa mashabiki wataipokea kwa mikono yote miwili, na pia wataifurahia kwani ni story inayoelezea maisha halisi ya Mtanzania" alisema Akim ambaye ni manager pia wa MASTER ARTS GROUP.

Filamu hiyo yenye matukio ya kusisimua inataraiwa kurekodiwa na TIMAMU EFFECTS kampuni ambayo ilitengeneza pia filamu ya DAMALISA, Akim alipoulizwa ni kwanini asifanye na kampuni nyingine tofauti na TIMAMU EFFECTS, alisema kuwa imani yake inamuonyeshakuwa bado hajapata kuona kampuni ya utengenezaji wafilamu ambayo itakidhi mahitaji yake kuanzia Quality ya picha mpaka editing...