TICO EDITOR

Monday, September 20, 2010

JUMA KILOWOKO SAJUKI AOKOA MAISHA YA MKEWE WASTARA

Hivi karibuni kumeibuka habari juu ya simu za maajabu ambazo zinasemekana kuleta madhara makubwa sana hapa Tanzania, awali mratibu wa mawasiliano nchini aliripoti kuwa hakuna uthibitisho wa aina yoyote juu ya swala hili na hivyo kumaanisha kwamba hakuna madhara ya aina yoyote katika matumizi ya vyombo vya mawasiliano hususani simu za mkononi, hivyo habari zinazoenezwa na baadhi ya watu kuhusu kutokea kwa madhara mara tu mtu anapopigiwa simu kwa namba ambazo hazieleweki mfano. 0000000000000000, mara tu anapopokea hupoteza maisha ama kupararaizi ni uzushi mtupu.

Katika hali isiyo ya kawaida hivi karibuni msanii wa maigizo Wastara Juma aliyewahi kutamba na filamu ya Mboni yangu, 2Brothers, Round, Vita Mkomanae, alipigiwa simu na moja kati ya namba hizo ambazo hazieleweki hivyo alimtaarifu mumewe Juma Kilowoko juu ya simu hiyo. ndipo mumewe alipokurupuka na kumpokonya simu mkewe na kumkataza asije akaipokea kwani anaweza kupoteza maisha au kupararaizi
Ingawa Wastara hakuonesha kuamini maneno hayo na kudai kuwa alitarajia kupokea simu kutoka nje ya nchi hivyo mara nyingi simu za kutoka nje huwa hazionyeshi namba ya mpigaji bali huwa inaonekana 'private no' or 'unknown call' hivyo kusababisha mabishano baina ya wapendanao hao wawili na mwisho kufikia muafaka wa kutoipokea simu hiyo...