TICO EDITOR

Monday, September 20, 2010

JACKSON KABIRIGI WA TANZANIA AFANANISHWA NA CHWENEYEGAYE (TSOTS) WA SOUTH AFRICA


Msanii wa filamu nchini Tanzania Jackson Kabirigi, aliyewahi kutamba katika filamu ya BORN TO SUFFER, MY NEPHEW, NUNDA na nyinginezo, hivi karibuni alijikuta akipigwa na butwaa baada ya baadhi ya mashabiki wake waliopo nchini Afica ya Kusini kumpachika jina la TSOTS wa BONGO,

"kiukweli nilishangaa sana na nilipochunguza kwanini wananifananisha na msanii huyo ambaye makazi yake ni nchini Africa ya Kusini, baadhi ya watu waliniambia kuwa kufananishwa kwangu kulitokana na jinsi nilivyoigiza katika filamu ya MY NEPHEW iliyofanywa nchini South Africa" alisema Jackson kabirigi.

Ndani ya filamu hiyo iliyorekodiwa na kuongozwa na RASHID MRUTU, pia kufanyiwa editing na TIMOTH CONRAD wa TIMAMU EFFECTS, wameshiriki waigizaji wakubwa kutoka nchini Africa Kusini, Botswana, Ghana, Uganda, Tanzania...