TICO EDITOR

Sunday, September 26, 2010

JACKSON KABIRIGI NA TIMOTH CONRAD

I'M A FIGHTER NI ZAIDI YA MY NEPHEW - JACKSON KABIRIGI



Jackson kabirigi aweka wazi kuwa filamu mpya anayoitengeneza kwa hivi sasa akiwa ndani ya kampuni ya TIMAMU EFFECTS ambayo ameipa jina la I'M A FIGHTER itakuja kufunika ile mbaya soko la filamu nchini.
akiielezea kwa ufupi filamu hiyo alisema ni filamu imbayo imegusa hisia zote hivyo kulingana na uwezo aliouonyesha ndani ya filamu hiyo anaamini kuwa ni zaidi ya kiwango alichokionyesha ndani ya filamu ambay iliwahi kutikisa vilivyo kunako market ya filamu zakibongo MY NEPHEW ilichezwa nchini Africa ya kusini na hapa nyumbani Mbeya Tanzania...

Friday, September 24, 2010

BONGO MOVIE MISTAKES

Timamu Effects imeanzisha kurasa ambayo itakuwa ikikuonyesha makosa ambayo yamekuwa yakifanyika katika baadhi ya filamu zetu zakitanzania (BONGO MOVIE MISTAKES), ndani ya page hiyo utapata kuona baadhi ya filamu zakitanzania ambazo zinamakosa ya wazi kabisa na yandani ambayo yamejificha...
Bonyeza hapa kuona filamu gani tumeichambua kwa wiki hii na makosa yake

Monday, September 20, 2010

BAADA YA DAMALISA SASA NI HIDEN TRUTH

Baada ya filamu ya DAMALISA kuingia sokoni na kupokelewa vizuri na mashabiki wa filamu za kutisha, sasa AKIM NATIBU ambaye ndiye aliyeiproduce filam hiyo ya DAMALISA, anaandaa filamu nyingine ambayo anatarajia itakuwa bomba kuliko DAMALISA.

Pia filamu hiyo ambayo ameipa jina la HARD TIME (Ukweli uliofichika), inatarajia kuanza kurekodiwa mara ifikapo mwezi 11 mwaka huu, "ni matarajio yangu kuwa mashabiki wataipokea kwa mikono yote miwili, na pia wataifurahia kwani ni story inayoelezea maisha halisi ya Mtanzania" alisema Akim ambaye ni manager pia wa MASTER ARTS GROUP.

Filamu hiyo yenye matukio ya kusisimua inataraiwa kurekodiwa na TIMAMU EFFECTS kampuni ambayo ilitengeneza pia filamu ya DAMALISA, Akim alipoulizwa ni kwanini asifanye na kampuni nyingine tofauti na TIMAMU EFFECTS, alisema kuwa imani yake inamuonyeshakuwa bado hajapata kuona kampuni ya utengenezaji wafilamu ambayo itakidhi mahitaji yake kuanzia Quality ya picha mpaka editing...

JUMA KILOWOKO SAJUKI AOKOA MAISHA YA MKEWE WASTARA

Hivi karibuni kumeibuka habari juu ya simu za maajabu ambazo zinasemekana kuleta madhara makubwa sana hapa Tanzania, awali mratibu wa mawasiliano nchini aliripoti kuwa hakuna uthibitisho wa aina yoyote juu ya swala hili na hivyo kumaanisha kwamba hakuna madhara ya aina yoyote katika matumizi ya vyombo vya mawasiliano hususani simu za mkononi, hivyo habari zinazoenezwa na baadhi ya watu kuhusu kutokea kwa madhara mara tu mtu anapopigiwa simu kwa namba ambazo hazieleweki mfano. 0000000000000000, mara tu anapopokea hupoteza maisha ama kupararaizi ni uzushi mtupu.

Katika hali isiyo ya kawaida hivi karibuni msanii wa maigizo Wastara Juma aliyewahi kutamba na filamu ya Mboni yangu, 2Brothers, Round, Vita Mkomanae, alipigiwa simu na moja kati ya namba hizo ambazo hazieleweki hivyo alimtaarifu mumewe Juma Kilowoko juu ya simu hiyo. ndipo mumewe alipokurupuka na kumpokonya simu mkewe na kumkataza asije akaipokea kwani anaweza kupoteza maisha au kupararaizi
Ingawa Wastara hakuonesha kuamini maneno hayo na kudai kuwa alitarajia kupokea simu kutoka nje ya nchi hivyo mara nyingi simu za kutoka nje huwa hazionyeshi namba ya mpigaji bali huwa inaonekana 'private no' or 'unknown call' hivyo kusababisha mabishano baina ya wapendanao hao wawili na mwisho kufikia muafaka wa kutoipokea simu hiyo...

JACKSON KABIRIGI WA TANZANIA AFANANISHWA NA CHWENEYEGAYE (TSOTS) WA SOUTH AFRICA


Msanii wa filamu nchini Tanzania Jackson Kabirigi, aliyewahi kutamba katika filamu ya BORN TO SUFFER, MY NEPHEW, NUNDA na nyinginezo, hivi karibuni alijikuta akipigwa na butwaa baada ya baadhi ya mashabiki wake waliopo nchini Afica ya Kusini kumpachika jina la TSOTS wa BONGO,

"kiukweli nilishangaa sana na nilipochunguza kwanini wananifananisha na msanii huyo ambaye makazi yake ni nchini Africa ya Kusini, baadhi ya watu waliniambia kuwa kufananishwa kwangu kulitokana na jinsi nilivyoigiza katika filamu ya MY NEPHEW iliyofanywa nchini South Africa" alisema Jackson kabirigi.

Ndani ya filamu hiyo iliyorekodiwa na kuongozwa na RASHID MRUTU, pia kufanyiwa editing na TIMOTH CONRAD wa TIMAMU EFFECTS, wameshiriki waigizaji wakubwa kutoka nchini Africa Kusini, Botswana, Ghana, Uganda, Tanzania...