TICO EDITOR

Thursday, December 23, 2010

FILAMU YA BRIEFCASE IMEINGIZWA KATIKA TUZO ZA MIN ZIFF

Filamu mpya ya briefcase iliyotengenezwa na kampuni ya WAJEY FILM ikishirikiana na TIMAMU EFFECTS zote za dar. imeonyesha record nzuri kimauzo tangu ilipoingia kunoko soko la filam nchini.
kutokana na ubora wa filamu hiyo yakitanzania iliyotengenezwa katika kisiwa cha zanzibar waandaaji wa tuzo za MIN ZIFF wameamua kuipendekeza ingiie katika kinyanganyiro cha kugombia tuzo ya filamu bora.
"Kwakweli najisikia vizuri sana kuona jinsi watu wanavyokubali na kuzipenda kazi zetu na mpaka kufikia hatua yakuipendekeza kuingia katika MIN ZIFF, na ninaimani itafanikiwa kuchukua tuzo hizo kutokana na ubora wafilamu yenyewe" alisema Wastara juma ambaye ndiye mtunzi wa filamu hiyo.
"mimi binafsi nilipopata habari ya filam yetu ya briefcase kuingia katika tuzo sikushtuka sana kwani nilikuwa namatarajio hayo, ila nilifurahi na kuishukuru sana crew ambayo nimekuwa nikifanya nayo kazi zetu pia namshukuru zaidi TIMOTH CONRAD ' TICO ' ambaye ndiye editor wa filam hiyo kwa uwezo wake mkubwa waubunifu kwani amechangia kwa kiasi kikubwa kuiboresha filamu hiyo..." alisema Juma kilowoko 'sajuki' alipokuwa akizungumza na Timamu effects news.
kupata habari zaidi juu ya filamu hiyo tafadhali tembelea www.timamu.webs.com