TICO EDITOR

Saturday, December 11, 2010

NIPO CHIMBO NAIUNDA VOLCANO - DENIS WA TEMPTATION

Denis Devid aliyewahi kung'ara katika filamu ya TEMPTATION aeleza wazi jinsi anavyoiunda volcano na kufafanua kuwa hana lengo la kuiangamiza dunia kwa volcano anayoitengeneza bali analengo lakuitetemesha tasnia ya filamu nchini baada ya kukaa kimya tangu alipotoka na filamu ya TEMPTATION.
"Kwakipindi kirefu nimekuwa kimya lakini nataka kuwaambia wadu kuwa nilikuwa chimbo nikipata mafunzo ya jinsi ya kuiunda volcano ambayo naamini itaitikisa tasnia ya filamu na kuwafanya wadau kuamini kuwa nililetwa duniani kwa lengo lakuushangaza ulimwengu" alisema Denis alipokuwa akiongea na TIMAMU EFFECTS.
Pia alipoulizwa ni ujio gani anatarajia kuja nao baada ya TEMTATION akasema kuwa "wadau watarajie vumbi katika FANS TOUR filamu mpya iliyotengenezwa kwa kiwango cha kimataifa chini ya kampuni ya MAGIC SCREEN iliyopo jijini Dar"