TICO EDITOR

Wednesday, December 15, 2010

QUEEN OF BONGO FILM KUFANYA BONGE LA SHOO SIKU YA CHRISMAS

Tarehe 25 mwezi wa 12 ndani ya jiji la mwanza kutakuwa na tukio lakihistoria ambapo quen of bongo film (WASTARA JUMA) akiambatana na wasanii kama Juma kilowoko, Z. Anton, H. baba, Zigamba pamoja na wasanii wengine wengi watatoa burudani kwa mashabiki wa jijini Mwanza ndani ya VIWANJA VYA CCM KIRUMBA...
"lengo lakufanya shoo hii ni kutaka kutoa burudani kwa mashabiki wetu, sababu tumegundua kuwa wapo wadau wetu wengi ndani ya jiji la mwanza na wanatamani japo siku moja wakutane na sisi ana kwa ana na kupata burudani LIVE" alisema Queen of bongo film (wastara Juma), pia Juma kilowoko ambaye pia atakuwepo na kutoa sapoti kubwa katika shoo hiyo inayotarajiwa kukata kiu ya burudani ya wakazi wa mwanza alisema kuwa huu ni mwanzo na kwamba mara watakapo maliza shoo hiyo jijini mwanza wanatarajia kuzunguka baadhi ya mikoa mingine ya hapa nchini ili pia kukonga nyoyo za mashabiki.
ndani ya shoo hiyo pia kutakuwa na burudani tofauti tofauti zikiwemo ngoma za asili kutoka kwa Zigamba akiwa na kundi lake, pia itashereheshwa na Z. Anton mzee wa kisiwa cha malavidavi, pamoja na H. Baba.
"kiukweli tunaisubiri kwa hamu kubwa shoo hiyo kwani tumekuwa tukitamani japo siku moja tuwaone sajuki na wastara kwa kweli tumekuwa tukinunua sana kazi zao na tunazipenda sana kwakweli" alisema shabiki mmoja wa burudani jijini mwanza...

TIMAMU EFFECTS INAWATAKIA BURUDANI NJEMA WAKAZI WA JIJI LA MWANZA