TICO EDITOR

Wednesday, May 25, 2011

RAMADHANI PII, UJIO WANGU NI ZAIDI YA RADI

Msanii chipukizi wa filamu Tanzania Ramadhani Pii ambaye ameshiriki katika filamu ya HOME VILLAGE ameongea na chanzo chetu cha habari hapo jana katika viwanja vya mwalimu nyerere dar-er-salam msanii huyo akiwa anatokea inchini kenya nairobi kwa ajili ya maandalizi ya filamu ya TARAFA YA WAFU filamu hiyo itayomkutanisha na wasanii mahiri wa hapa nchini Tanzania kama Omary Clayton,Denis David,Jackson Kabirigi,Dady na wengine wengi,PII amesema kuwa amejiandaa vizuri sana kuonyesha uwezo wa kimataifa na kuwapa ratha watanzania

UMOJA WA WANA TIMAMU EFFECTS NDIO SIRAHA YAO

Kampuni maarufu ya kuandaa filamu inchini Tanzania TIMAMU EFFECTS wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kazi nzito,msemaji mkuu wa kampuni hiyo bw. Timoth Conrad amesema kuwa umoja na ushirikiano walionao ndio moja ya siraha yao katika utendaji wakazi na kuongeza kuwa wamewaandalia watanzania kazi ambayo itakuwa ni utambulisho wa ujio mpya kabisa tofauti na kazi ambazo wamezifanya awali,ni filamu iitwayo HOME VILLAGE ambayo ipo katika hatua za mwisho kuingia sokoni,amemaliza kwa kuwashukuru watanzania kwa ushirikiano ambao wanauonyesha na kuwaomba waendelee kuwa makini katika kuangalia kazi ambazo zinafaa zenye mafundisho na zenye kuzingatia maadili.

DADY RAMADHANI BACK FROM JO'BURG CITY TO HOME VILLAGE

Msani maarufu DADY RAMADHANI kutoka S.AFRICA na kwasasa yupo inchi Tanzania kwa ajiri ya kushiriki katika filamu ya HOME VILAGE ambayo meshirikiana na wasanii mahili wa hapa inchini Tanzania akiwemo msanii JACKSON KABIRIGI,DENIS DAVID,OMARY CLAYTON,LATIFA IDABU na wengine wengi,filamu hiyo ikiwa tayari kwa ajiri ya kuingia sokoni DADY amesema kuwa watanzania watarajie filamu yenye ubora wa kimataifa na kuwa ahidi kuwa kwasasa bado yupo Tanzania kwa ajili ya kufanya mapinduzi katika tasnia hii ya filamu Tanzania.

HOME VILLAGE SASA TAYARI KUINGIA SOKONI

Kwa wale wadau na wapenzi wa filamu Tanzania waliokuwa wakisubilia kwa hamu sana filamu ya HOME VILLAGE baada ya kuyaona matangazo mengi katika vyombo vya habari mbalimbali sasa ipo tayari kuingia sokoni,filamu hiyo ambayo imewakutanisha wasanii kutoka ndani na nje ya tanzania,kazi hiyo ambayo inatarajiwa kufanya vizuri na kuleta mapinduzi katika tasnia ya filamu Tanzania,
Baada ya kufanya kazi kwa nguvu lengo lilikuwa ni moja tu kufanya kazi itakayopokelewa na wapenzi wa filamu kwa mikono miwili, na kukubali kuwa watu wanafanya kazi bila kuwa na masihara, sisi yaani mimi na crew yangu ya Timamu tumekusudia kuleta mapinduzi ya vitendo na si maneno” Anasema Bob Jack

Thursday, May 19, 2011

KIUNGO KIPYA NDANI YA TIMAMU EFFECTS

IBRAHIM LUHIZO nikijana wa kitanzania mwenye umri mdogo sana ila mwenye uwezo na kipaji kikubwa katika uandaaji wa filamu ambaye kwa sasa amejiunga na kampuni kubwa nchini tanzania TIMAMU EFFECTS ikiwa ni moja ya kujiongezea uwezo na uzoefu kutoka kwa wataalamu kama TIMOTH CONRAD,editor huyo IBRA ambaye ameanza kuonyesha uwezo wake katika filamu iitwayo MUMIANI ambayo inatarajiwa kuingia sokoni hivi karibuni,amesema kuwa amefurahi sana kujiunga na kampuni kubwa ya TIMAMU EFFECTS anaimani atafanya kazi kwa ufanisi wa hari ya juu na kuleta mabadiliko katika soko la filamu Tanzania,na amewasii watanzania kuwa wawe waangalifu na makini katika kuchagua filamu za kuangalia na si kuchagua majina ya watu maarufu.

OMARY CLAYTON KUJADILIWA NA MASTAA WAKUBWA

Msanii OMARY CLAYTON  kijana alieanza sanaa ya maigizo tangu akiwa na umri mdogo sana katika kikundi cha Kaole sanaa group nyota yake ilianza kung'ara pale alipoteuliwa katika wasanii walioshiriki katika tamthilia ya FUNIKO vilevile akiwa bado yupo kaole akachaguliwa kushiriki tamthilia ya TETEMO,Omary alionyesha uwezo mkubwa sana kiasi cha kuzikonga nyoyo za watanzania wengi na kujizolea mashabiki rukuki ndani na nje ya Tanzania,baada ya hapo alijiunga mojakwamoja na uigizaji wa firamu na kupata nafasi ya kucheza firamu ya WICKED LOVE ya msanii Vicent Kigosi akiwa ndani ya uigizaji akapata ujuzi wa uandishi wa story za movie ambapo alianza na story SHAKIRA ambayo ilichezwa na Vicent Kigosi pamoja na Iren Uwoya,baada ya hapo Omary aliandika story ya movie iitwayo HEKIMA na kuicheza mwenyewe akishirikiana na wasanii kama Hemedi Suleimani,Wastara Juma,Juma Kilowoko movie ambayo imefanya vizuri sana katika soko la filamu Tanzania kiasi cha kuwafanya mastaa wakubwa kukaa vikao vya kujadili kuhusu mapinduzi aliyoyafanya msanii OMARY CLAYTON ambaye kwasasa anapatikana katika filamu ya HOME VILLAGE ambayo pia imeongeza mjadala mkubwa katika tasnia ya filamu Tanzania,msanii Omary amesema kuwa yeye kwa sasa amejiunga na kampuni ya TIMAMU EFFECTS kwa ajili ya kuleta mabadiliko katika tasnia ya filamu na kuwa yuko tayari kupambana na wote wanaotaka kumrudisha nyuma pia amewataka wadau wa filamu nje na ndani ya Tanzania kukaa tayari kuipokea HOME VILLAGE.

HATUA YA KIMATAIFA

Ni baada ya ukimya wa muda mrefu sasa Jackson Kabirigi aka mzee wa hisia ukipenda unaweza kumuita Nunda ambae ni director,akiwa pamoja na Denis David ama wengi wamemzoeya kama mzee wa Tampetion wakiwa katika picha ya pamoja ambayo inautambulisha ujio wao mpya kabisa katika filamu ya HOME VILLAGE ambayo ipo karibuni kuingia sokoni ikiwa imewakutanisha wasanii mbalimbali wa nje na ndani ya tanzania.Kama vile msanii Dady Ramadhani kutoka South Africa ambaye ametamba katika filamu ya MY NEPHEW MONEY TRANSFER ambaye amefanya vizuri katika HOME VILLAGE.vilevile katika filamu ya HOME VILLAGE utakutana na wasanii wengine wa hapa nchini kama vile Omari Clayton ambaye kwa sasa anatamba na filamu ya HEKIMA,Latifa Idabu,Sabrina Omary na wengine wengi,filamu ya HOME VILLAGE ni filamu ambayo imefanywa katika ubora wa kimataifa na inatarajiwa kureta mapinduzi makubwa katika soko la filamu ndani na nje ya Tanzania,msemaji mkuu wa kampuni ya TIMAMU EFFECTS ambayo ndio imeiandaa filamu hiyo bw.Timoth Conrad ambae pia ndio camera man na editor wa filamu hiyo amesema kuwa watanzania watarajie kupata kitu ambacho kitawaonyesha kuwa sasa kweli Tanzania kuna waandaaji wa filamu zenye ubora wa kimataifa,kazi kwako wewe mdau na mpenzi wa filamu Tanzania.

MAHESABU MAKALI

Timoth conrady aka TICO camera man na editor anae tikikisa soko la filamu ndani na nje ya tanzania akiwa katika moja ya kazi,ameeleza kuwa mahesabu ni muhimu sana katika swala zima la utendaji wa kazi yake,akiwa katika maandalizi ya filamu ya HOME VILLAGE filamu ambayo imezuwa gumzo sokoni ikiwa hata bado haijatoka rasmi amesema kuwa filamu hiyo ameifanya katikka mazingira magumu sana kutokana na mahitaji ya story kuwa katika uhalisia halisi hivyo ilimbidi atumie mahesabu makali katika kuhakikisha anaitendea haki filamu hiyo ambayo ipo karibuni kuingia sokoni,kama unavyomuona TICO katika picha yupo kwenye mahesabu.