TICO EDITOR

Saturday, June 4, 2011

SANAA YA BONGO ILI IKUWE YAHITAJI KUJITUMA,DADY

Msanii DADY RAMADHANI kutoka S.A ambaye kwa sasa yuko nchini tanzania kwa ajiri ya kukamilisha baadhi ya movie,amesema kuwa sanaa ya hapa tanzania inahitaji kujituma sana ili iweze kuleta ushindani na mataifa mengine ambayo kwa sasa yamefika mbali na kuwafanya wasanii wenyewe kunufaika na kazi zao tofauti na hapa nchini msanii bado ana hali duni,DADY amesema kazi ambazo amefanya mpaka sasa moja tayari imekamilika na ipo tayari kuingia sokoni wiki hii ambayo ni filamu ya home village pia amesema kuwa filamu hiyo ataleta mabadiliko sana kutokana na jinsi ambavyo wasanii wamejituma na kufanya kitu ambacho bilashaka kitaleta mabadiliko katika tasnia hii ya filamu tanzania

Wednesday, May 25, 2011

RAMADHANI PII, UJIO WANGU NI ZAIDI YA RADI

Msanii chipukizi wa filamu Tanzania Ramadhani Pii ambaye ameshiriki katika filamu ya HOME VILLAGE ameongea na chanzo chetu cha habari hapo jana katika viwanja vya mwalimu nyerere dar-er-salam msanii huyo akiwa anatokea inchini kenya nairobi kwa ajili ya maandalizi ya filamu ya TARAFA YA WAFU filamu hiyo itayomkutanisha na wasanii mahiri wa hapa nchini Tanzania kama Omary Clayton,Denis David,Jackson Kabirigi,Dady na wengine wengi,PII amesema kuwa amejiandaa vizuri sana kuonyesha uwezo wa kimataifa na kuwapa ratha watanzania

UMOJA WA WANA TIMAMU EFFECTS NDIO SIRAHA YAO

Kampuni maarufu ya kuandaa filamu inchini Tanzania TIMAMU EFFECTS wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kazi nzito,msemaji mkuu wa kampuni hiyo bw. Timoth Conrad amesema kuwa umoja na ushirikiano walionao ndio moja ya siraha yao katika utendaji wakazi na kuongeza kuwa wamewaandalia watanzania kazi ambayo itakuwa ni utambulisho wa ujio mpya kabisa tofauti na kazi ambazo wamezifanya awali,ni filamu iitwayo HOME VILLAGE ambayo ipo katika hatua za mwisho kuingia sokoni,amemaliza kwa kuwashukuru watanzania kwa ushirikiano ambao wanauonyesha na kuwaomba waendelee kuwa makini katika kuangalia kazi ambazo zinafaa zenye mafundisho na zenye kuzingatia maadili.

DADY RAMADHANI BACK FROM JO'BURG CITY TO HOME VILLAGE

Msani maarufu DADY RAMADHANI kutoka S.AFRICA na kwasasa yupo inchi Tanzania kwa ajiri ya kushiriki katika filamu ya HOME VILAGE ambayo meshirikiana na wasanii mahili wa hapa inchini Tanzania akiwemo msanii JACKSON KABIRIGI,DENIS DAVID,OMARY CLAYTON,LATIFA IDABU na wengine wengi,filamu hiyo ikiwa tayari kwa ajiri ya kuingia sokoni DADY amesema kuwa watanzania watarajie filamu yenye ubora wa kimataifa na kuwa ahidi kuwa kwasasa bado yupo Tanzania kwa ajili ya kufanya mapinduzi katika tasnia hii ya filamu Tanzania.

HOME VILLAGE SASA TAYARI KUINGIA SOKONI

Kwa wale wadau na wapenzi wa filamu Tanzania waliokuwa wakisubilia kwa hamu sana filamu ya HOME VILLAGE baada ya kuyaona matangazo mengi katika vyombo vya habari mbalimbali sasa ipo tayari kuingia sokoni,filamu hiyo ambayo imewakutanisha wasanii kutoka ndani na nje ya tanzania,kazi hiyo ambayo inatarajiwa kufanya vizuri na kuleta mapinduzi katika tasnia ya filamu Tanzania,
Baada ya kufanya kazi kwa nguvu lengo lilikuwa ni moja tu kufanya kazi itakayopokelewa na wapenzi wa filamu kwa mikono miwili, na kukubali kuwa watu wanafanya kazi bila kuwa na masihara, sisi yaani mimi na crew yangu ya Timamu tumekusudia kuleta mapinduzi ya vitendo na si maneno” Anasema Bob Jack

Thursday, May 19, 2011

KIUNGO KIPYA NDANI YA TIMAMU EFFECTS

IBRAHIM LUHIZO nikijana wa kitanzania mwenye umri mdogo sana ila mwenye uwezo na kipaji kikubwa katika uandaaji wa filamu ambaye kwa sasa amejiunga na kampuni kubwa nchini tanzania TIMAMU EFFECTS ikiwa ni moja ya kujiongezea uwezo na uzoefu kutoka kwa wataalamu kama TIMOTH CONRAD,editor huyo IBRA ambaye ameanza kuonyesha uwezo wake katika filamu iitwayo MUMIANI ambayo inatarajiwa kuingia sokoni hivi karibuni,amesema kuwa amefurahi sana kujiunga na kampuni kubwa ya TIMAMU EFFECTS anaimani atafanya kazi kwa ufanisi wa hari ya juu na kuleta mabadiliko katika soko la filamu Tanzania,na amewasii watanzania kuwa wawe waangalifu na makini katika kuchagua filamu za kuangalia na si kuchagua majina ya watu maarufu.

OMARY CLAYTON KUJADILIWA NA MASTAA WAKUBWA

Msanii OMARY CLAYTON  kijana alieanza sanaa ya maigizo tangu akiwa na umri mdogo sana katika kikundi cha Kaole sanaa group nyota yake ilianza kung'ara pale alipoteuliwa katika wasanii walioshiriki katika tamthilia ya FUNIKO vilevile akiwa bado yupo kaole akachaguliwa kushiriki tamthilia ya TETEMO,Omary alionyesha uwezo mkubwa sana kiasi cha kuzikonga nyoyo za watanzania wengi na kujizolea mashabiki rukuki ndani na nje ya Tanzania,baada ya hapo alijiunga mojakwamoja na uigizaji wa firamu na kupata nafasi ya kucheza firamu ya WICKED LOVE ya msanii Vicent Kigosi akiwa ndani ya uigizaji akapata ujuzi wa uandishi wa story za movie ambapo alianza na story SHAKIRA ambayo ilichezwa na Vicent Kigosi pamoja na Iren Uwoya,baada ya hapo Omary aliandika story ya movie iitwayo HEKIMA na kuicheza mwenyewe akishirikiana na wasanii kama Hemedi Suleimani,Wastara Juma,Juma Kilowoko movie ambayo imefanya vizuri sana katika soko la filamu Tanzania kiasi cha kuwafanya mastaa wakubwa kukaa vikao vya kujadili kuhusu mapinduzi aliyoyafanya msanii OMARY CLAYTON ambaye kwasasa anapatikana katika filamu ya HOME VILLAGE ambayo pia imeongeza mjadala mkubwa katika tasnia ya filamu Tanzania,msanii Omary amesema kuwa yeye kwa sasa amejiunga na kampuni ya TIMAMU EFFECTS kwa ajili ya kuleta mabadiliko katika tasnia ya filamu na kuwa yuko tayari kupambana na wote wanaotaka kumrudisha nyuma pia amewataka wadau wa filamu nje na ndani ya Tanzania kukaa tayari kuipokea HOME VILLAGE.

HATUA YA KIMATAIFA

Ni baada ya ukimya wa muda mrefu sasa Jackson Kabirigi aka mzee wa hisia ukipenda unaweza kumuita Nunda ambae ni director,akiwa pamoja na Denis David ama wengi wamemzoeya kama mzee wa Tampetion wakiwa katika picha ya pamoja ambayo inautambulisha ujio wao mpya kabisa katika filamu ya HOME VILLAGE ambayo ipo karibuni kuingia sokoni ikiwa imewakutanisha wasanii mbalimbali wa nje na ndani ya tanzania.Kama vile msanii Dady Ramadhani kutoka South Africa ambaye ametamba katika filamu ya MY NEPHEW MONEY TRANSFER ambaye amefanya vizuri katika HOME VILLAGE.vilevile katika filamu ya HOME VILLAGE utakutana na wasanii wengine wa hapa nchini kama vile Omari Clayton ambaye kwa sasa anatamba na filamu ya HEKIMA,Latifa Idabu,Sabrina Omary na wengine wengi,filamu ya HOME VILLAGE ni filamu ambayo imefanywa katika ubora wa kimataifa na inatarajiwa kureta mapinduzi makubwa katika soko la filamu ndani na nje ya Tanzania,msemaji mkuu wa kampuni ya TIMAMU EFFECTS ambayo ndio imeiandaa filamu hiyo bw.Timoth Conrad ambae pia ndio camera man na editor wa filamu hiyo amesema kuwa watanzania watarajie kupata kitu ambacho kitawaonyesha kuwa sasa kweli Tanzania kuna waandaaji wa filamu zenye ubora wa kimataifa,kazi kwako wewe mdau na mpenzi wa filamu Tanzania.

MAHESABU MAKALI

Timoth conrady aka TICO camera man na editor anae tikikisa soko la filamu ndani na nje ya tanzania akiwa katika moja ya kazi,ameeleza kuwa mahesabu ni muhimu sana katika swala zima la utendaji wa kazi yake,akiwa katika maandalizi ya filamu ya HOME VILLAGE filamu ambayo imezuwa gumzo sokoni ikiwa hata bado haijatoka rasmi amesema kuwa filamu hiyo ameifanya katikka mazingira magumu sana kutokana na mahitaji ya story kuwa katika uhalisia halisi hivyo ilimbidi atumie mahesabu makali katika kuhakikisha anaitendea haki filamu hiyo ambayo ipo karibuni kuingia sokoni,kama unavyomuona TICO katika picha yupo kwenye mahesabu.

Saturday, April 30, 2011

Wednesday, March 30, 2011

BECA AWASHUKURU WADAU KWAKUMPOKEA VIZURI

Msanii wa kizazi kipya bakari hassan au beca awashukuru watanzania kwa kuipokea vizuri video yake mpya ya natumaini remix.
"kwa kweli napata farijiko kila nikiona simu yangu inaita na kati ya simu 50 ambazo nazopokea kwa siku simu 30 sinakuwa nizapongezi juu ya video ya wimbo wangu wa natumaini" alisema beca alipozungumza na TIMAMU EFFECTS

Monday, March 28, 2011

HEKIMA HIYOOOO!!!!!

film mpya inayokwenda kwa jina la HEKIMA inatarajia kuingia kunako masoko hivi karibuni...

Friday, March 4, 2011

HEKIMA YAMTENGUA MKONO OMARY CLAYTON

Omary clayton maarufu kama omy aliyewahi kung'aa katika drama (michezo ya luningani) kupitia kaole sanaa group, na pia aliwahi kushiriki katika baadhi ya filamu kadhaa hapa nchini kama The killers, Home Village, na nyingine nyingi ambazo bado hazijaingia kunako masoko.
     hivi karibuni nusura apate kilema cha maisha kwa kuvunjika mkono alipokuwa akicheza filam mpya itakayokwenda kwa jina la HEKIMA, iliyowashirikisha wasanii wenye uwezo katika fani ya uigizaji, sakata hilo lilitokea pale ambapo Omy alipokuwa akicheza na Hemed suleiman.
"kiukweli pamoja na kuigiza lakini nilipata kipigo cha ukweli kutoka kwa hemedi nilipocheza kama amenifuma nikiwa na mkewe (wastara), mwanzoni nilidhani kwamba hemed alikuwa anafanya kusudi lakini nilikuja kugundua kuwa ule ulikuwa ni  mzuka wa kazi hivyo sikugombana nae zaidi nilimshukuru kwa kunipa sapoti ya kutosha kupelekea mimi kucheza katika uhalisia" alisema Omary alipoulizwa baada ya kumaliza kucheza scene hiyo.
     kwa upande wake hemed alisema kuwa dogo ni muelewa ndomana hakuweza kupanik nilipomuumiza kwani anajua hizi ni kazi so haipaswi kupaniki na yeye anaelewa mizuka ya kazi ilivyo.
"lakini pia nashukuru mungu anaendelea vizuri na mkono wake umerejea katika hali yake ya kawaida niko peace na mshkaji hatuna bifu maana watu wakisikia mimi na omy tumegombana wataanza kuzusha bifu" alimalizia Hemed
katika kuthibitisha hilo hemed alipiga picha ya pamoja na Omy ili kuondoa tofauti zao.

HAPA OMARY CLAYTON AKIWA NA HEMED BAADA YA SCENE HIYO

TIMAMU EFFECTS inampa pole omy na kumwambia kuwa akaze buti ndo kazi lakini pia tunawaambia mashabiki wa filam kuwa wakae mkao wa kula kuisubiri filamu hiyo ya aina yake iliyoshirikisha wasanii kama WASTARA JUMA, HEMED SULEIMAN, JUMA KILOWOKO, MAINDA SUKA, CHARLES MAGARI, OMARY CLAYTON, pamoja na hao wakali kushiriki pia filam hiyo imeongozwa na OMARY na kupigwa picha na KABUTI ONYANGO kutoka katika kampuni ya JML PRODUCTION.

Friday, February 25, 2011

HOME VILLAGE SASA IPO JIKONI

 Hapa kazi ikiendelea
 Denis David naye amepata nafasi yakuonyesha kipai chke
 Mi nawaita maembe  ya TIMAMU EFFECTS Jackson na Denis
 Hili ni zao jipya  katika tasnia ya filam anaitwa ANGEL naye ameonyesha ujuzi ndani ya HOME VILLAGE
Bashiri production designer wetu naye ameshiriki
Mwanadada ANGEL yupo kazini
Badra akiwa katika moja ya scene za filam hiyo
The Best cameraman in TZ TIMOTH CONRAD au wengi wanapenda kumuita TICO akiwa kazini
Yani full mauaji ndani ya HOME VILAGE
kazi kama kawa
Rashid mrutu naye alikuwepo location kutoa 'sapoti'
hapa baada ya kutoka kupiga scene moja ngumu sana
JEMBEEE anaitwa HAMISI CHECHE wakazi wa mabibo wanamfahamu maana ndiye mtemi wao naye ameshiriki katika filam hii
TICO TICOLA KAMA KAWA
Moja ya scene ngumu alizocheza bashiri bashirima
duu jack kwa kujituma tuu hajambo
JEMBEEE wanamuita 50 cent sijui kwanini lakini naye ameshiriki
hapa tuko pamoja 
full shangwe ikifika jioni tukiwa kambini kwetu kwa mzee joto
 Usister duu kando hapa kazi kwanza
duu ebwana tulichoka kinoma

Friday, February 4, 2011

FILAMU MPYA YA 077 DAYS NUSURA IMTENGUE KIUNO SAJUKI

JUMA KILOWOKO (SAJUKI) AKIUGULIA BAADA YA KUUMIA WAKATI WA UTENGENEZAJI WA FILAMU YA 077 DAYS
 HAPA AKIPATIWA HUDUMA YA KWANZA
 AKIJARIBU KUNYANYUKA 
HAPA AKITABASAMU MARA BAADA YA KUPATA NAFUU



TIMAMU EFFECTS KUTOA ZAWADI KWA WADAU

Kampuni ya utengenezaji wa filamu nchini Tanzania TIMAMU EFFECTS chini ya uongozi wa TIMOTH CONRAD (TICO) editor aliyewafanya baadhi ya ma-editor wa filam za kitanzania kurudi shule baada ya kugundua kuwa kuna baadhi ya vitu bado hawajavijua ambavyo wamekuwa wakiviona katika kazi ambazo zimefanywa na TICO akiwa ndani ya kampuni hiyo ya TIMAMU EFFECTS.

Bila shaka jina la filamu kama VITA ambayo imewakutanisha wasanii maarufu kama vile juma kilowoko{sajuki}wastara,mwisho mwampamba ambaye alikuwa ni mshiriki wa BBA{big brother africa}denis sweya{dino}na wengine wengi hiyo ni moja wapo ya kazi zilizofanyika katika kampuni hiyo,vilelevile kuna kazi kama MY NEPHEW filamu ambayo imetikisa sana soko la filamu ndani na nnje ya tanzania pia imekutanisha wasanii mahiri kama jackson kabiligi{bob jack} doki,na wasanii kutoka nnchini botswana na south africa ambako ndiko ilipochezewa filamu hiyo,pia kuna filamu inayokwenda kwa jina la THE KILLER ambayo ilipokelewa kwa mikono yote miwili sokoni,kiukweli mpaka sasa ukitamka neno TIMAMU EFFECTS bila shaka kwa wale wadau na wapenzi wa filamu tanzania na nje ya tanzania moja kwa moja wanaelewa unaongelea kampuni ambayo inafanya kazi katika ubora wa kimataifa na utakumbuka kazi kama ,DAMALISA,na BRIFCASE.

Kampuni hiyo ambayo kwasasa ipo mbioni kuachia filamu kazaa ambazo ziko tayari na baadhi zikiwa mbioni kukamilika kazi hizo ni pamoja na RED & GREEN,THE SKENDO,HOME VILLAGE ni filamu ambazo zinatarajiwa kuleta mapinduzi ya ukweli katika tasnia hii ya filamu tanzania.


Director, editor na cameraman TIMOTH CONRAD baada ya kupokea pongezi kutoka kwa wadau na wapenzi wa filamu tanzani yeye pamoja na crew nzima ya kampuni ya TIMAMU EFFECTS wameamua kutoa special thanx kwa wadau na wapenda filamu za kutisha hapa nchini kwa kuandaa filamu mpya ya kutisha itakayoitwa HOME VILLAGE,
kwa sasa crew nzima ipo location katika kuikamilisha filamu hiyo ya aina yake na ambayo haijawahi kutokea bongo...

Wednesday, January 26, 2011

WASTARA, SAJUKI, YUSUF MLELA, DINNO WATEMBELEA WATOTO YATIMA JIJINI MWAMZA

 HAMIDA GENIUS AKIPATA CHAKULA CHA MCHANA PAMOJA NA WATOTO YATIMA JIJINI MWANZA
 JAMAA ANAITWA SENJERE NAYEYE ALIKUWEPO KUTOA BURUDANI
 UKITAZAMA VIZURI UTAMUONA WASTARA, YUSUF MLELA NA WENGINE KATIKA PICHA YA PAMOJA
 TUCHEZE PAMOJA JAMANI SISI NIWAMOJA DEFFERENT COLOR ONE PEOPLE
 
 BAADA YA SHUGULI KUISHA
 KUSHOTO NI DINO KULIA NI YUSUF MLELA
 JUMA KILOWOKO
 TUKO PAMOJA
 MLELA NA SAJUKI
 WASTARA AKITUMBUIZA
DINO AKIMNONG'ONEZA KITU SAJUKI