Thursday, December 23, 2010
SIKUWAHI KUOTA KUWA MUIGIZAJI - JACKSON KABIRIGI
JACK aliyewahi kutamba katika filam za Born to suffer, Nunda, My nephew, Cross Roads ameiambia Timamu effects habari kuwa katika maisha yake amekuwa akiwaza kuja kuwa msanii wakuigiza tofauti na watu wanavyodhani kuwa yeye alikuwa na ndoto za kuwa msanii wakuigiza ndio maana anafanya vizuri katika kila kazi anayopea kushiriki.
"kipindi naingia dar nilikuja kwa lengo moja tu kupeleka nyimbo zangu redioni na kuzipromot kisha kuanza kusambaza albamu yangu niliyoirekodia nchini uganda, lakini sikufanikiwa hata kidogo hivyo nikaambulia kujiingiza katika sanaa ya uigizaji" alisema Jackson katika waraka wa histori ya maisha yake aliouanika katika mtandao wa timamu effects news...
JACKSON KABIRIGI NI ZAIDI YA ACTOR - AKIM
"kwakweli licha ya kwamba jackson ni rafiki yangu lakini lakini pia ndiye mtu ninaeamini anaweza kufanya kila kitu ambacho atahitajika kukifanya katika kazi ya kuigiza" alisema Akim alipokuwa akizungumza na timamu effects news wakati wakiwa location wakiendela na shooting ya filamu mpya itakayokwenda kwa jina la HARD TIME.
FILAMU YA BRIEFCASE IMEINGIZWA KATIKA TUZO ZA MIN ZIFF
kutokana na ubora wa filamu hiyo yakitanzania iliyotengenezwa katika kisiwa cha zanzibar waandaaji wa tuzo za MIN ZIFF wameamua kuipendekeza ingiie katika kinyanganyiro cha kugombia tuzo ya filamu bora.
"Kwakweli najisikia vizuri sana kuona jinsi watu wanavyokubali na kuzipenda kazi zetu na mpaka kufikia hatua yakuipendekeza kuingia katika MIN ZIFF, na ninaimani itafanikiwa kuchukua tuzo hizo kutokana na ubora wafilamu yenyewe" alisema Wastara juma ambaye ndiye mtunzi wa filamu hiyo.
"mimi binafsi nilipopata habari ya filam yetu ya briefcase kuingia katika tuzo sikushtuka sana kwani nilikuwa namatarajio hayo, ila nilifurahi na kuishukuru sana crew ambayo nimekuwa nikifanya nayo kazi zetu pia namshukuru zaidi TIMOTH CONRAD ' TICO ' ambaye ndiye editor wa filam hiyo kwa uwezo wake mkubwa waubunifu kwani amechangia kwa kiasi kikubwa kuiboresha filamu hiyo..." alisema Juma kilowoko 'sajuki' alipokuwa akizungumza na Timamu effects news.
kupata habari zaidi juu ya filamu hiyo tafadhali tembelea www.timamu.webs.com
Wednesday, December 15, 2010
NIMEOKOKA KIKWELI JAPO WATU HAWANIAMINI - Mainda
"Mimi sio machepele na kusema kweli nakerwa sana na kitendo cha baadhi ya watu kunibeza kwa kitendo changu cha kutangaza kwamba nimeokoka, sijui kwa nini watu hawaniamini?" alisema Mainda alipokuwa akizungumza na Timamu Effects ndani ya viwanja vya Ledaz jijini dar.
QUEEN OF BONGO FILM KUFANYA BONGE LA SHOO SIKU YA CHRISMAS
"lengo lakufanya shoo hii ni kutaka kutoa burudani kwa mashabiki wetu, sababu tumegundua kuwa wapo wadau wetu wengi ndani ya jiji la mwanza na wanatamani japo siku moja wakutane na sisi ana kwa ana na kupata burudani LIVE" alisema Queen of bongo film (wastara Juma), pia Juma kilowoko ambaye pia atakuwepo na kutoa sapoti kubwa katika shoo hiyo inayotarajiwa kukata kiu ya burudani ya wakazi wa mwanza alisema kuwa huu ni mwanzo na kwamba mara watakapo maliza shoo hiyo jijini mwanza wanatarajia kuzunguka baadhi ya mikoa mingine ya hapa nchini ili pia kukonga nyoyo za mashabiki.
ndani ya shoo hiyo pia kutakuwa na burudani tofauti tofauti zikiwemo ngoma za asili kutoka kwa Zigamba akiwa na kundi lake, pia itashereheshwa na Z. Anton mzee wa kisiwa cha malavidavi, pamoja na H. Baba.
"kiukweli tunaisubiri kwa hamu kubwa shoo hiyo kwani tumekuwa tukitamani japo siku moja tuwaone sajuki na wastara kwa kweli tumekuwa tukinunua sana kazi zao na tunazipenda sana kwakweli" alisema shabiki mmoja wa burudani jijini mwanza...
TIMAMU EFFECTS INAWATAKIA BURUDANI NJEMA WAKAZI WA JIJI LA MWANZA
Saturday, December 11, 2010
NIPO CHIMBO NAIUNDA VOLCANO - DENIS WA TEMPTATION
"Kwakipindi kirefu nimekuwa kimya lakini nataka kuwaambia wadu kuwa nilikuwa chimbo nikipata mafunzo ya jinsi ya kuiunda volcano ambayo naamini itaitikisa tasnia ya filamu na kuwafanya wadau kuamini kuwa nililetwa duniani kwa lengo lakuushangaza ulimwengu" alisema Denis alipokuwa akiongea na TIMAMU EFFECTS.
Pia alipoulizwa ni ujio gani anatarajia kuja nao baada ya TEMTATION akasema kuwa "wadau watarajie vumbi katika FANS TOUR filamu mpya iliyotengenezwa kwa kiwango cha kimataifa chini ya kampuni ya MAGIC SCREEN iliyopo jijini Dar"
SAJUKI NA STARA KUJA NA 077 DAYS
077 Day’s imetayarishwa na kampuni ya Wajey Film Company ikishirikiana na Timamu Effects zote za jijini Dar es Salaam, filamu hiyo inaongelea mambo ya miujiza ambayo yaliwahi kutokea miaka ya nyuma, ni filamu ambayo inatarajiwa kuwa ya aina yake kwa sababu ya mfumo wa hadithi ulivyotumika na wasanii jinsi walivyocheza kwa hisia huku ikiwa imerekodiwa nje ya jiji la Dar es Salaam, akiongea na FC Sajuki alisema.
“Filamu hii nategemea ilete mapinduzi makubwa kabisa katika tasnia hii ya filamu na wapenzi wangu wenyewe wanajua uwezo wetu katika sanaa, na mfano mliuona katika filamu iliyopita na kufanya vizuri sana ya Vita Mkomanae hadi kuweza kuchukua tuzo kwa mwaka huu, tuzo hii kwetu sisi Wajey Film Company imekuwa chachu ya kufanya kazi kwa nguvu”
Alimalizia kwa kuongea Sajuki ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa Kampuni hiyo.
Filamu hii imeandikwa na Timoth Conrad na kuongozwa na Juma Kilowoko (Sajuki) akishirikiana na Timothy Condard (Tico), wasanii walioshiriki ni Nassoro Ndambwe ( Zigamba) Wastara Juma , Juma Kilowoko na wasanii wengine nyota na wakali, filamu hiyo ipo studio katika hatua za mwisho katika uhariri, na inatarajia kutoka hivi karibuni.
Friday, December 10, 2010
JACKSON KABIRIGI APANIA KUFANYA MAKAMUZI KATIKA RUGS BEGINNING...
"japokuwa watu wamekuwa wakinikubali hasa kutokana na uwezo wakiuchezaji ambao nimekuwa nikiuonyesha katika baadhi ya filam ambazo nimewahi kushiriki, kwa sasa nataka kuwaonyesha zaidi watanzania na watu wengine Africa na dunia nzima kuwa nilizaliwa kuja kuushangaza ulimwengu" alisema jackson kabirigi
pia aliongeza kuwa ndani ya film hiyo ambayo nayeye pia ni mmoja kati ya jupo la watunzi wa filam hiyo itakuja kuwashitua watazamaji ambao wamekuwa wakidhani kuwa 'wazungu' pekee ndio wanaweza kutengeneza movie ambayo itamfanya mtazamani asinyanyuke mara anapoanza kuitaza.
"sihitaji kuongea mengi sana ila waingoje kazi kwa hamu" alisema jackson kwa kujiamini...
TUMEFUNGUA BLOG MPYA www.timamu.webs.com
bonyeza hapa kutembelea blog yetu mpya www.timamu.webs.com
'ENJOY YOUR SELF'
Monday, December 6, 2010
077 DAYS is Coming soon...
pia filamu hiyo imeshirikisha wasanii wenye uwezo na kazi zao kama Juma kilowoko (sajuki), Wastara Juma, Nassoro Ndambwe, Zigamba na wengine wengi...
hii ni crew iliyoshiriki kuikamilisha filam hiyo
Story: Timoth Conrad, Wastara juma
Camera/editing: Timoth conrad (Tico)
location manager: Nassor Ndambwe
Make up & costume: Wastara juma
visual effects: Timoth conrad (Tico)
Director: Juma kilowoko (sajuki)
Asst. Director: Timoth Conrad (Tico)
click here to watch 077 trailer>>
Sunday, October 17, 2010
FILAMU MPYA YA CROSS ROAD IKO NJIANI
Sunday, September 26, 2010
I'M A FIGHTER NI ZAIDI YA MY NEPHEW - JACKSON KABIRIGI
Jackson kabirigi aweka wazi kuwa filamu mpya anayoitengeneza kwa hivi sasa akiwa ndani ya kampuni ya TIMAMU EFFECTS ambayo ameipa jina la I'M A FIGHTER itakuja kufunika ile mbaya soko la filamu nchini.
akiielezea kwa ufupi filamu hiyo alisema ni filamu imbayo imegusa hisia zote hivyo kulingana na uwezo aliouonyesha ndani ya filamu hiyo anaamini kuwa ni zaidi ya kiwango alichokionyesha ndani ya filamu ambay iliwahi kutikisa vilivyo kunako market ya filamu zakibongo MY NEPHEW ilichezwa nchini Africa ya kusini na hapa nyumbani Mbeya Tanzania...
Friday, September 24, 2010
BONGO MOVIE MISTAKES
Bonyeza hapa kuona filamu gani tumeichambua kwa wiki hii na makosa yake
Monday, September 20, 2010
BAADA YA DAMALISA SASA NI HIDEN TRUTH
Pia filamu hiyo ambayo ameipa jina la HARD TIME (Ukweli uliofichika), inatarajia kuanza kurekodiwa mara ifikapo mwezi 11 mwaka huu, "ni matarajio yangu kuwa mashabiki wataipokea kwa mikono yote miwili, na pia wataifurahia kwani ni story inayoelezea maisha halisi ya Mtanzania" alisema Akim ambaye ni manager pia wa MASTER ARTS GROUP.
Filamu hiyo yenye matukio ya kusisimua inataraiwa kurekodiwa na TIMAMU EFFECTS kampuni ambayo ilitengeneza pia filamu ya DAMALISA, Akim alipoulizwa ni kwanini asifanye na kampuni nyingine tofauti na TIMAMU EFFECTS, alisema kuwa imani yake inamuonyeshakuwa bado hajapata kuona kampuni ya utengenezaji wafilamu ambayo itakidhi mahitaji yake kuanzia Quality ya picha mpaka editing...
JUMA KILOWOKO SAJUKI AOKOA MAISHA YA MKEWE WASTARA
Katika hali isiyo ya kawaida hivi karibuni msanii wa maigizo Wastara Juma aliyewahi kutamba na filamu ya Mboni yangu, 2Brothers, Round, Vita Mkomanae, alipigiwa simu na moja kati ya namba hizo ambazo hazieleweki hivyo alimtaarifu mumewe Juma Kilowoko juu ya simu hiyo. ndipo mumewe alipokurupuka na kumpokonya simu mkewe na kumkataza asije akaipokea kwani anaweza kupoteza maisha au kupararaizi
Ingawa Wastara hakuonesha kuamini maneno hayo na kudai kuwa alitarajia kupokea simu kutoka nje ya nchi hivyo mara nyingi simu za kutoka nje huwa hazionyeshi namba ya mpigaji bali huwa inaonekana 'private no' or 'unknown call' hivyo kusababisha mabishano baina ya wapendanao hao wawili na mwisho kufikia muafaka wa kutoipokea simu hiyo...
JACKSON KABIRIGI WA TANZANIA AFANANISHWA NA CHWENEYEGAYE (TSOTS) WA SOUTH AFRICA
"kiukweli nilishangaa sana na nilipochunguza kwanini wananifananisha na msanii huyo ambaye makazi yake ni nchini Africa ya Kusini, baadhi ya watu waliniambia kuwa kufananishwa kwangu kulitokana na jinsi nilivyoigiza katika filamu ya MY NEPHEW iliyofanywa nchini South Africa" alisema Jackson kabirigi.
Ndani ya filamu hiyo iliyorekodiwa na kuongozwa na RASHID MRUTU, pia kufanyiwa editing na TIMOTH CONRAD wa TIMAMU EFFECTS, wameshiriki waigizaji wakubwa kutoka nchini Africa Kusini, Botswana, Ghana, Uganda, Tanzania...